Jiometri

Jiometria inajulisha ukubwa wa pembetatu.

Jiometri (pia: Jiometria, kutoka neno la Kigiriki γεωμετρία, geometria, linaloundwa na geo- "dunia" na -metron "kipimo", kwa kupitia Kiingereza geometry) ni tawi la hisabati linalochunguza ukubwa, mjao, umbo na mahali pa eneo au gimba.

Tawi la jiometri linalochunguza pembetatu hasa huitwa trigonometria.

Maumbo huwa na nyanda (dimensioni) mbili yakiwa bapa, au tatu kama ni gimba. Kwa mfano mraba, pembetatu na duara ni bapa na kuwa na nyanda 2 za upana na urefu. Kumbe tufe (kama mpira) au mchemraba huwa na nyanda 3 za upana, urefu na kimo (urefu kwenda juu).


Jiometri

Dodaje.pl - Ogłoszenia lokalne