Yesu kutolewa hekaluni ni tukio la utoto wake, siku arubaini baada ya kuzaliwa, iliyopangwa na Torati kuwa siku ya kumtakasa mama yeyote aliyemzaa mtoto wa kiume.
Siku hiyo aliletwa na Yosefu na Maria katika hekalu la Yerusalemu ili atolewe kwa Mungu, akiwa mtoto wa kiume wa kwanza, akakombolewa kwa sadaka ya fukara. Ndipo alipotambuliwa na kutangazwa na wazee wawili watakatifu, Simeoni na Anna.