Barua kwa Tito ni kimojawapo kati ya vitabu 27 vya Agano Jipya katika Biblia ya Kikristo.
Pamoja na barua mbili kwa Timotheo inaunda kundi la Nyaraka za Kichungaji. Mada za hizo zote ni mafundisho sahihi ya imani na uadilifu wa matendo yanayofuatana nayo.
Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.