Our website is made possible by displaying online advertisements to our visitors.
Please consider supporting us by disabling your ad blocker.

Responsive image


Uumbaji

Uumbaji ni tendo linalosadikika analiweza Mwenyezi Mungu tu kwa sababu ni kusababisha kitu kuwepo kutoka utovu wa vyote.

Hivyo vitu vyote vimeanza kuwepo kwa uwezo wake tu, ingawa kwa kawaida vinatokana na vile vilivyotangulia (k.mf. wazazi).

Kwamba kiumbe kimeweza kikatokana na vingine namna hiyo haifuti ukweli kwamba kimeanza na kinaendelea kuwepo kwa uwezo wa Muumba aliyesababisha viumbe hivyo viwepo na kuzaa au kubadilika.

Kwa msingi huo, si lazima dhana ya mageuko ya spishi ipingane na imani katika uumbaji.


Previous Page Next Page