Utoaji mimba au Uavyaji wa mimba ni tendo la hiari la kuua mimba iliyokwishatungwa tumboni mwa mwanamke. Unaweza kufanywa naye au na watu wengine kwa kibali chake au bila ya hicho.
Sababu zinaweza kuwa mbalimbali: hatari kwa uhai wa mjamzito, haya kwa tendo lililotunga mimba kinyume cha maadili, hali ya uchumi, ulemavu wa mama au wa mimba, ubaguzi wa jinsia n.k.
Ni tofauti na tukio lisilokusudiwa la mimba kuharibika kwa sababu mbalimbali.