Our website is made possible by displaying online advertisements to our visitors.
Please consider supporting us by disabling your ad blocker.

Responsive image


Sifongo-bahari

Sifongo-bahari
Sifongo kijani (Aplysina aerophoba)
Sifongo kijani (Aplysina aerophoba)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia
Nusuhimaya: Parazoa
Faila: Porifera
Ngazi za chini

Ngeli 4:

Muundo wa sifongo-bahari; njano: pinakositi, nyekundu: koanositi, kijivu: mesohili, samawati: mtiririko wa maji.

Sifongo-bahari ni wanyama sahili wa maji (bahari na baridi) katika faila Porifera (maana: walio na vinyweleo) ambao wamekazika chini, ijapokuwa spishi chache zinaweza kwenda kwa mbio wa mm 1-4 kwa siku. Spishi nyingi sana zina umbo wa yai, bonge au bomba. Kuna kipenyo kikubwa kiasi juu yao (osculum au kidomo) na vinyweleo vidogo vingi (ostia) kila sehemu ya mwili.

Mwili wa sifongo ni ukuta wa seli tu ambao unazunguka uwazi wa katikati. Ukuta huu umeumbwa kwa tabaka la kolajini (collagen) au mesohili (mesohyl) lililofunikwa na seli nje na ndani. Hata vinyweleo vimezungukwa na seli zinazoitwa porositi (porocytes). Seli zenye kijeledi (flagellum), ambazo huitwa koanositi (choanocytes), zisukuma maji kuelekea osculum na maji mengine yaingia kupitia ostia. Chembe za kulika zilizomo majini ziliwa kwa phagocytosis.


Previous Page Next Page






Sponsdier AF ሰፍነግ AM إسفنجيات Arabic اسفنجيات ARZ স্পঞ্জ AS Porifera AST Süngərlər AZ Болоттар BA Губкі BE Губкі BE-X-OLD

Responsive image

Responsive image