Our website is made possible by displaying online advertisements to our visitors.
Please consider supporting us by disabling your ad blocker.

Responsive image


Papa Gregori I

Papa Gregori I.
Gregori akishughulikia muziki mtakatifu.
Mchoro wa Andrea Mantegna juu ya Gregori akiwa na Yohane Mbatizaji, Benedikto wa Nursia na Jeromu.
Papa Gregori I.
Kaburi la Gregori I, ndani ya Basilika la Mt. Petro huko Vatikano.

Papa Gregori I (Roma, Italia, takriban 540 – Roma, 12 Machi 604) alikuwa Papa kuanzia 3 Septemba 590 hadi kifo chake[1].

Alimfuata Papa Pelagio II akafuatwa na Papa Sabinian.

Jina lake la kuzaliwa pia lilikuwa Gregorius. Kutokana na umuhimu wake katika historia, hasa ya Kanisa na ya Italia, aliongezewa lile la Magnus, yaani "Mkuu".

Lakini mwenyewe, aliposikia kuwa Patriarki wa Konstantinopoli alijiita "Patriarki wa ekumene", aliitikia kwa kujiita "Servus servorum Dei" (yaani "Mtumishi wa watumishi wa Mungu"), jina linalotumiwa hata leo na kila Papa. Akijali umoja wa kidugu katika Kanisa lote, yeye aliona unyenyekevu unatakiwa kuwa adili la msingi la kila askofu kama lilivyokuwa kwa Kristo aliyetuosha miguu. Jina hilo alilojichagulia lilidhihirisha kabisa namna yake ya kuishi na kutenda.

Hamu yake ilikuwa kuishi kweli kama mmonaki, akizama daima katika Neno la Mungu, lakini kwa kumpenda alijifunza kuwa mtumishi wa wote katika nyakati za tabu.

Hivyo akawa mchungaji bora katika kuongoza Kanisa, katika kusaidia kwa hali na mali wenye shida, katika kustawisha maisha ya kimonaki na katika kuimarisha na kueneza kotekote imani, akiandika kwa ajili hiyo vitabu maarufu vya maadili na uchungaji[2].

Tangu zamani anaheshimiwa kama mtakatifu na babu wa Kanisa.

Mwaka 1298 Papa Bonifasi VIII alimuongezea sifa ya mwalimu wa Kanisa.

Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 3 Septemba[3].

  1. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  2. https://www.santiebeati.it/dettaglio/24350
  3. Martyrologium Romanum

Previous Page Next Page