Mende | ||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Mende
| ||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
| ||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||
Oda ya chini 1 ya mchwa; familia za juu 3 na familia 9 za mende:
|
Mende au kombamwiko ni wadudu wadogo hadi wakubwa kiasi wa oda ya Blattodea (blatta = mende, eidos = umbo). Tangu mwanzo wa karne hii wataalamu wengi wamesadiki kwamba mchwa ni aina za mende wa kijamii[1][2]. Kwa hivyo oda yao, Isoptera, huwekwa ndani ya Blattodea kama oda ya chini mara nyingi. Kuna maainisho mengine pia[3]. Kundi la mchwa linajadiliwa katika ukurasa wake.
Kuna zaidi ya spishi 4,000 za mende, kati yao 30 hupatikana kwenye makazi ya watu, huku nne kati yao zinafahamika kama wadudu wasumbufu.
Miongoni mwa spishi zinazofahamika sana ni mende wa Amerika, ambaye ana urefu wa milimita 30, mende wa Ujerumani mwenye urefu wa milimita 15, na mende wa Asia anayekaribia urefu wa milimita 25. Mende wa kisasa ni wakubwa kidogo kuliko mende wa kale.