Mbege ni kileo asili cha Wachagga, wakazi wa mkoa wa Kilimanjaro.
Mbege hutengenezwa kwa ndizi mbivu, kimea cha ulezi, na maji.
Mara nyingi mbege hutengenezwa na wanawake na hutumika katika sherehe na matukio mbalimbali kama vile harusi, misiba, kipaimara, kuzaliwa kwa mtoto, n.k. Mbege hutumiwa pia kama faini kwenye mahakama za jadi. Utengenezaji wa mbege hufanywa pia kwa biashara. Hapo huuzwa katika vilabu vya pombe na pia nyumbani.