Haki ya kuishi inatokana na imani kwamba binadamu ana haki ya kuishi na haswa, hapaswi kuuawa na mtu au kitu kingine, ikiwa pamoja na serikali. Dhana ya haki ya kuishi inatokana na mijadala juu ya masuala ya adhabu ya kifo, vita, utoaji mimba, kifo cha hiari, ukatili wa polisi, mauaji wakati wa kujihami, na kwa wengine hata haki za wanyama. Baadhi ya watu hawakubaliani juu ya maeneo ambayo kanuni hii inatumika, pamoja na masuala kama haya yaliyoorodheshwa hapo awali.