Daraja takatifu katika madhehebu mbalimbali ya Ukristo ni jina la vyeo vya askofu, kasisi na shemasi vinavyounda uongozi wa Kanisa.
Katika Kanisa Katoliki na ya Waorthodoksi ngazi hizo tatu zinaunda kwa pamoja mojawapo ya sakramenti saba ambazo Yesu Kristo alizianzisha na kulikabidhi Kanisa lake.
Baadhi ya Waprotestanti wana huduma hizo lakini kwao si sakramenti.