Akko (kwa Kiebrania: עַכּוֹ, ʻAkkō; pia: Akka (kwa Kiarabu: عكّا, ʻAkkā[1]; uliwahi kuitwa pia: Tolemais) ni mji wa pwani katika Israeli Kaskazini. Una bandari asili katika Hori ya Haifa.[2]
Kutokana na umuhimu wa mahali ulipo, umekaliwa na watu mfululizo tangu zama za Shaba hadi leo,[3] ingawa uliwahi kuangamizwa mara kadhaa.
Wakazi wa sasa ni 48,000 hivi.
Mwaka 58 Mtume Paulo alikaa siku moja na Wakristo wa huko mwishoni mwa safari yake ya tatu ya kimisionari, akielekea Yerusalemu (Mdo 21:7)
Umeorodheshwa na UNESCO kati ya mahali pa Urithi wa Dunia.
Ni pia makao makuu ya dini ya Bahai.