Our website is made possible by displaying online advertisements to our visitors.
Please consider supporting us by disabling your ad blocker.

Responsive image


Agano Jipya

Agano Jipya

Agano Jipya ni sehemu ya pili ya Biblia ya Kikristo, ikifuata Agano la Kale: Agano Jipya limefichika katika lile la Kale, na Agano la Kale limedhihirika katika lile Jipya.

Linakusanya vitabu ambavyo Wakristo wote wanaviheshimu kama vitakatifu na vilivyoandikwa baada ya ujio wa Yesu Kristo hadi mwisho wa wakati wa mitume wake.

Vitabu vyake 27 vinaleta habari zake, za mitume wake na za mwanzo wa Kanisa lake.

Vinatakiwa kusomwa kama kilele cha ufunuo wa Mungu kwa binadamu kadiri ya Historia ya Wokovu.

Jina lilitungwa na nabii Yeremia (Yer 31:30) alipotambua kwamba kwa kiasi fulani lile la mlima Sinai lilikuwa na dosari (Eb 8), lakini Mungu kwa uaminifu wake asingeweza kukubali likome tu.

Vitabu vya Agano Jipya ni kama ifuatavyo (Kwa mabano: kifupi cha kawaida kwa kutaja kitabu hiki).


Previous Page Next Page






Nuwe Testament AF አዲስ ኪዳን AM Nīwu Gecȳþnes ANG العهد الجديد Arabic ܕܝܬܝܩܝ ܚܕܬܐ ARC العهد الجديد ARZ Nuevu Testamentu AST ЦӀияб КъотӀи AV Əhdi-cədid AZ عهد جدید AZB

Responsive image

Responsive image